Featured

    Featured Posts

LOWASSA AIBUKIA KAHAMA KWA WAHANGA WA MGODI WALIOISHI KWA KULA MENDE NA VYURA SIKU 41 ARDHINI

Mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA Edward Lowassa leo ametoa shilingi Milioni 2 kwa wahanga waliookolewa katika mgodi wa Nyangalata wanaopatiwa matibabu katika hospitali ya halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga.
Akikabidhi fedha hizo kwa wahanga hao, Lowassa amesema ametoa fedha hizo kama msaada ili ziwasaidie kwa matibabu kwa muda wote watakapokuwa hospitalini hapo, ambapo kila mmoja amepatiwa shilingi laki tano.
Mmoja wa wahanga hao, Joseph Burule amesema kitendo cha Lowassa kuwatembelea hospitalini hapo kimewapa faraja kubwa, kwani tangu waokolewe na kuanza kupatiwa matibabu hakuna kiongozi mkubwa aliyefika kuwajulia hali pamoja na kuwapa pole.
Burule amesema kitendo hicho kinatakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa viongozi pindi linapotokea jambo la kusikitisha kama hilo, na kusema kuwa fedha hizo zitawasaidia kujikimu hospitalini hapo.
Kwa upande wake Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Shinyanga kupitia CHADEMA Salome Makamba amewaambia wananchi waliojitoza kumsabahi Lowassa kuwa, Lowassa amekuja kuwapa pole wahanga hao na hakuja kwa masuala ya kisiasa.
Novemba 15, 2015 wahanga 5 kati ya 6 waliofukiwa na kifusi katika machimbo ya nyangalata wilayani kahama waliopolewa wakiwa hai baada ya kukaa ndani ya mashimo kwa siku 41, ambapo jana mmoja kati yao amefariki dunia.
Ni hivi karibuni baada ya kuokolewa mmoja wa wahanga hao alikaririwa akimuulizia Lowassa kama alishinda urais Tanzania kwenye uchaguzi na baada ya kuambiwa hakushinda alikosa raha.

Maromboso wa Yamoto band kaamua kuvuta jiko na ndoa ilifungwa juzi kimya kimya Tazama picha za Tukio zima hapa Ziko hapa

MASIKITIKO: NAPE NNAUYE YAMTOKEA HAYA



NAPE NNAUYE APATA AJALI MBAYA LINDI
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amepata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea jijini Dar es Salaam.

TAZAMA PICHA HIZI ZA MICHEZO HII YA AJABU DUNIANI


Devotees of the Chinese Samkong shrine and the Chinese Ban Tha Rue shrine walked through Phuket yesterday in a procession that worships abstinence from meatMany of the men wore garlands of flowers around their necks while they shoved multiple items - including serrated metal bars - through their cheeksMeanwhile, a man wearing a green and gold outfit dribbled as he forced the ends of ten knives through one of his cheeks

A young man with intricate tattoos on his shoulders pierces one of his cheeks with two oddly-shaped daggersSo

Afumaniwa, ajitosa baharini

Chande abdallah na issa mnally
AIBU! Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Zuhura maarufu kama Lolo Princessa ambaye ni mpenzi wa kijana anayejulikana kama Koko Byanco juzikati alijikuta akipata aibu kubwa baada ya kufumaniwa akiwa na mwanaume mwingine kiasi cha kusababisha mchepuko huo kujitosa baharini katika ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam kukwepa kipigo.
Tukio hilo lililotokea mchana kweupe na kuwastaajabisha watu, lilitokea jioni ya Oktoba 14 mwaka huu, wakati Watanzania wakiwa mapumzikoni kukumbuka siku ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kilichotokea miaka 16 iliyopita jijini London, Uingereza.
Mapema, dawati la Oparesheni Fichua Maovu (OFM) lilipata taarifa kutoka kwa Koko, akilalamika kuwa amenasa meseji kwenye simu ya mtu wake, ikionyesha mawasiliano na mwanaume mwingine, wakipeana ahadi ya kukutana ufukweni siku hiyo, ambazo zilikuwa na viashiria vyote vya kimahaba.
Koko alidai kwa muda mrefu, mwenzake huyo anayeishi naye Mabibo jijini Dar, alikuwa na tabia ya kuendekeza michepuko bila kujali kuwa wanatarajia kufunga ndoa Novemba mwaka huu na mara kwa mara amekuwa akiwalalamikia mashemeji zake lakini wamekuwa wakimuona muongo.
“Mpaka nimeamua kuja kwenu nataka mnisaidie jamani maisha yangu hayana amani kabisa, naomba mnisaidie nimnase mbaya wangu na hii tabia ikome kwa wote wenye mambo kama hayo. Mbaya zaidi kwao hawajui kama ananisumbua, hivi nataka mashemeji zangu wamuone ndugu yao anachonifanyia,” alisema Koko.
Koko aliwakusanya shemeji zake na OFM ikiongozana na wanausalama, waliondoka kuelekea Coco Beach ambako baada ya msako mkali miongoni mwa mamia ya watu waliokuwa ‘wakila bata’, walifanikiwa kuwaona wawili hao wakiwa wamekaa pembeni peke yao wakiendelea kujinafasi.
Baada ya kuwaona huku makamanda wa OFM wakianza kukusanya ushahidi kwa kupiga picha, mwanaume alishindwa kuvumilia na kuanzisha timbwili kali kwa mgoni wake, ambaye alipoona ‘jeshi’ kubwa likimsogelea, alilazimika kukimbilia ndani ya bahari huku akifukuzwa na mwenye mali.
Baada ya mchepuko kukimbia, Koko alirejea kwa Lolo na kuendeleza mashambulizi, ambayo hata hivyo yalidhibitiwa na mashemeji waliotaka suala hilo kumalizwa kwa mazungumzo. Katika utetezi wake, Lolo alidai aliamua kujifariji ufukweni kwa vile mara nyingi mpenziwe huyo hujifanya yuko bize, hoja ambayo haikukubaliwa kuwa kigezo cha kuchepuka.

NYUMBA YA MWENYEKITI MWENZA WA UKAWA JAMES MBATIA YATEKETEA KWA MOTO


Yadaiwa kuwa sababu ni hitilafu ya umeme

Nyumba ya makazi ya mwenyekiti wa chama cha NCCR-MAGEUZI,JAMES MBATIA,imeteketea kwa moto jana majira ya saa saba unusu mchana , kwa kile kilichoelezwa kuwa huenda ni hitilafu ya umeme unaosemekana kukatika asubuhi na kurejea mchana kwa kasi zaidi.

Akizungumza ,kaka wa James Mbatia FELIX KESSI,amesema hadi sasa wanachoweza kueleza ni uharibifu uliotokea kutokana na moto huo , kwani hawakuwepo wakati wa tukio , ingawa anawashukuru majirani walioweza kuokoa baadhi ya vitu vya ndani.

Amesema ni mapema mno kuzungumzia aina ya uharibifu kwani atakayeweza kujua zaidi ni mkewe na Mbatia ambae kwa wakati huo, haikuweza kuzungumza naye, kufuatia kupandwa na shinikizo la damu kutokana na tukio hilo .

Kwa upande wake mkuu wa oparesheni hiyo kutoka kikosi cha zima moto na uokoaji kwa wakati huo nyumbani hapo sajenti HAJI MADULIKA, amesema kikosi chake kiliwahi eneo la tukio ingawa kutokana na ukubwa wa moto, walishindwa kuokoa baadhi ya vitu, aidha ameoneshwa kushangazwa kwake na tabia ya watu kuwashutumu askari wa zimamoto kwa kuchelewa huku wanacnhi wakielewa hali halisi ya barabara.
CHANZO: CHANNEL TEN

Paroko aacha swali gumu msiba wa Filikunjombe

Aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe enzi za uhai wake

PAROKO wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Epifania Kijichi, Dar es Salaam,  Respis Mzena, amehoji matukio ya watu wengi hasa wanasiasa kufa katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu kama ni mapenzi ya Mungu.
Paroko huyo alihoji hayo wakati akiongoza ibada ya kuaga mwili wa aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe na wenzake wawili, waliokufa katika ajali ya helikopta iliyotokea Alhamisi jioni katika Pori la Akiba la Selous.
Mbali na marehemu Filikunjombe, wengine waliopoteza maisha na kuagwa pamoja ni Plasdus Haule na Egid Nkwera ambao walikuwa watu wake wa karibu.
Mwingine aliyepoteza maisha katika ajali hiyo ni rubani wa helikopta hiyo, Kapteni William Silaa, ambaye ni baba mzazi wa Meya wa Manispaa ya Ilala anayemaliza muda wake Jerry Silaa.
Akitoa mahubiri katika ibada ya kumuombea marehemu, Paroko huyo alisema matukio ya vifo vya wanasiasa mwaka huu yanashangaza sana.
“Uchaguzi wa mwaka huu kuna nini hasa? kipindi hiki watu wanakufa sana kila siku huyu kafa huyu kafa…kwanini watu wanakufa sana? Hii ni mipango ya Mungu kweli?” alihoji Paroko huyo.
Akimuongelea marehemu Filikunjombe, alisema ni mtu aliyekuwa akijali na kupenda watu wote ambapo alitoa maisha yake katika kutumikia watu bila kujali itikadi zao.
Paroko huyo ambaye alisoma na Filikunjombe Seminari, alisema Serikali ingekuwa na wabunge wachapakazi 30 kama alivyokuwa Filikunjombe, nchi ingepiga hatua kubwa kwa sababu wakati wote alionekana akiwa jimboni kwake akisaidiana na wananchi katika shughuli mbalimbali.
Awali viongozi mbalimbali na wananchi wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete waliaga miili ya marehemu hao.
Akisoma salamu za rambirambi kutoka kambi rasmi ya upinzani, mgombea ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini kupitia NCCR-Mageuzi, David Kafulila alisema taifa limepoteza mbunge wa mfano.
Akitoa salamu kutoka CCM, Mbunge wa Bumbuli ambaye anatetea nafasi yake, January Makamba alisema chama kimepokea msiba huo kwa masikitiko makubwa na kimepoteza kiongozi ambaye kwa kauli zake na vitendo, aliwakumbusha nini hasa namna ya kuwa kiongozi wa CCM na kuwa mwana CCM.
Spika wa Bunge, Anne Makinda akitoa salamu za rambirambi kutoka bungeni, alisema Filikunjombe alikuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wote pamoja na kuwa bungeni kwa miaka mitano lakini mambo aliyoyafanya ni kama mtu aliyekaa zaidi ya miaka 20.

MFAHAMU MDADA MWANAHARAKATI ALIE AMUA KUJITANGAZA KUA AMEATHIRIKA NA UKIMWI NA KUBADILI MTAZAMO WA WENGI KUHUSU UGONJWA HUO.


Bi Phindile Sithole-Spong, mdada aliyejitangaza kua ameathrika na ukimwi.

Kama anavyo onekana kwenye picha hapo juu, Bi Phindile Sithole-Spong ni mwanaharakati kutoka Afrika Kusini anayeishi na virusi vya Ukimwi, amekuwa akiongoza juhudi za kukabiliana na unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi na hususan miongoni mwa vijana.
Mwanamke huyu aligundua akiwa na miaka kumi na tisa kwamba alizaliwa na ugonjwa wa Ukimwi, Phindile alijihusisha na usambazaji wa ujumbe kuhusu Ukimwi na Afya ya Uzazi, hasa maeneo ya kusini mwa Afrika, ambayo yameathirika pakubwa na Ukimwi.
Bi Sithole-Spong, alizindua kampeni ya Rebranding HIV mwaka 2013 kubadili mtazamo wa jamii kuhusu virusi vya Ukimwi, hasa miongoni mwa vijana akiwa katika chuo kikuu cha Cape Town.
Nchini Afrika Kusini takriban asilimia 11.2 ya raia wote wanaishi na virusi vya Ukimwi.
Kwa sasa, Bi Sithole-Spong ni mshauri wa mashirika makubwa ya kimataifa kama vile Muungano wa Afrika na UNAIDS.

Bi Phindile Sithole-Spong.

Baada ya kufahamu kuwa watu wa rika lake, familia na marafiki walikuwa wameathirika na janga la Ukimwi duniani pamoja na kuongezeka kwa maambukizi mapya nchini Afrika Kusini, licha ya kampeni mbalimbali, Phindile amekuwa akijihusisha na kampeni ya kuendeleza mtazamo chanya kuhusu Ukimwi na Afya ya Uzazi.
''Nina fahari sana moyoni kwa vijana ambao hawaaibiki kuishi na Ukimwi. Sote tunakumbwa na Ukimwi kila siku kama vijana, huwezi kutambua kama mtu ana Ukimwi au la, ni kama tu magonjwa mengine kwa sababu unaweza kujitibu,” anasema.
Kwa harakati zake za kuhamasisha mtazamo mwema kwa watu katika jamii zinazoathirika na janga la Ukimwi, amepongezwa sana.
“Ninafanya kitu ambacho ninakipenda sana. Huwa sihisi kwamba ni kazi. Sijilazimishi. Kwa mfano huwa siandiki hotuba zangu,” anasema.
"Huwa zinatoka katika sehemu halisi moyoni mwangu ambayo ina hamu ya kutaka kusaidia. Ya kutaka kupaza sauti yangu popote inapoweza.”

 
Bi Phindile Sithole-Spong.

Mwongozo mpya wa matibabu ya UKIMWI toka WHO,

Logo ya Shirika la Afya Duniani (WHO).

Shirika la Afya Duniani (WHO) limebadili msimamo wake wa awali ambapo walioathirika na virusi vinavyosababisha ukimwi (HIV) ilibidi wasubiri kuwa wagonjwa kabisa kabla ya kuanza kutumia tembe za kupunguza makali ya ukimwi.
WHO limeagiza kuwa kila mtu anayethibitishwa kuwa ameambukizwa na virusi vinavyosababisha ukimwi, HIV, anapaswa kuanza kupewa matibabu mara moja.
Mwongozo huu mpya unatokana na ushahidi unaoonyesha kuwa watu walio na HIV wanaoanza kutibiwa mara moja huishi kwa muda mrefu zaidi.
WHO linaamini kuwa mwongozo huu mpya unaweza kupunguza vifo zaidi ya milioni 21 kwa muda wa miongo miwili ijayo.


ARVS, dawa za kupunguza makali ya UKIMWI.

Ushahidi uliopatikana katika mataifa yanayostawi kama vile Marekani uanonyesha kuwa wagonjwa wengi wanaoanza kutibiwa tu mara wanapogunduliwa kuwa na virusi vya ukimwi huishi muda mrefu zaidi.
Shirika hilo pia linapendekeza kwamba makundi ya watu ambao wako katika hatari kubwa ya kuambukizwa wanapaswa kupewa nafasi ya kwanza kutibiwa hata kabla ya uchunguzi kufanywa.
Muongozo mpya uliotolewa unamaanisha kuwa watu milioni 37 kote duniani ambao wanauguwa UKIMWI wanapaswa kupewa dawa za kupunguza makali ya ukimwi
Kwa sasa, watu milioni 15 tu ndio wanapata dawa hizo kote duniani.
Ushauri wa shirika hilo umeungwa mkono na mashirika ya kutoa misaada ya matibabu.
Hata hivyo shirika hilo limesema kuwa kutibu wagonjwa wengi wapya kutahitaji fedha za ziada.

SOMA KISA CHA KUSIKITISHA CHA WAPENZI HAWA


Hii ni keki waliyojitengenezea wapenzi hawa wakimaanisha mpka kifo kiwatenganishe ndo wataachana,



HIKI NDO KILICHOMTOKEA MAROMBOSO SIKU YA BIRTHDAY YAKE

 
This was happened on Maromboso Birthday you will be shocked when you see this photo's what friend and family member did to him!!



SOMA KISA CHA MTOTO ALIYELIWA NA MBWA 12 KISHA KUFARIKI HUKO MKOANI MWANZA

Mtoto mmoja mkazi wa Malimbe jijini Mwanza aliyefahamika kwa jina la Jovina Rwegasira, 7, (pichani) aliyekuwa akisoma kwenye Kituo cha Chekechea cha ABC Malimbe, amefariki dunia baada ya kuvamiwa na mbwa 12 kisha kung’atwa hadi kufa baada ya kunyofolewa sehemu mbalimbali za mwili wake.
 Jovina Rwegasira enzi za uhai wake.
Akizungumza na gazeti hili mama mzazi wa mtoto huyo, Chausiku Haruna alisema mtoto wake aling’atwa na mbwa hao baada ya kutumwa na msichana wa kazi kwenda dukani kununua mafuta ya kupikia Septemba 18, mwaka huu.
“Wakati tukio linatokea mimi nilikuwa kazini kwani kazi yangu ni kuwapikia chakula mafundi ujenzi, sasa siku hiyo hawakuwepo ikabidi nirudi nyumbani.
“Nilipofika maeneo ya Vanesa karibu na nyumbani kwangu niliona watu wamejazana huku wakishangaa, baada ya kufika nikaambiwa mwanangu ameliwa na mbwa mpaka amefariki dunia, nikahisi kuchanganyikiwa ikabidi nisogee nikaone, nikakuta kweli mwanangu amefariki dunia,” alisema mama huyo.
Aliongeza kuwa ilibidi polisi waitwe, walipofika waliuchukua mwili wa mwanangu na kuupeleka hospitali kwa uchunguzi.
Mama wa marehemu.
“Marehemu alifikishwa kwenye Kituo cha Afya cha Igogo kilichopo wilayani Nyamagana na madaktari walithibitisha alikwisha fariki dunia ndipo ukapelekwa kuhifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando,” alisema.
Majirani walisema kwamba mbwa hao waliomuua mtoto huyo wanaishi kwenye msitu ambao uko karibu na Chuo cha Sauti Malimbe jijini hapa na hawana mwenyewe kutokana na chuo kufungwa, hawapati chakula hivyo kumtafuna mtoto huyo.
Baada ya tukio hilo, wananchi waliingia katika msituni huo na kuwasaka wanyama hao ambapo walifanikiwa kuwaua zaidi ya mbwa 60.

MAGUFULI AZURU KABURI LA SOKOINE

Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Pombe Magufuli akiweka shada kwenye kaburi la Waziri Mkuu wa zamani, Edward Moringe Sokoine, Monduli Juu.Mke wa Sokoine na binti yake (amabaye ni mgombea ubunge wa Jimbo la Monduli kwa tiketi ya CCM, Namelock Sokoine) wakiweka shada kwenye kaburi hilo.Magufuli akicheza ngoma ya kabila la Kimasai.

Mchungaji Gwajima Apewa Siku 14 za Kumfufua Kaka Yake Au Kupandishwa Kizimbani

Shamma Gwajima (kulia) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kushoto ni Raphah Gwajima.
********* ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, ametumiwa waraka mzito na wanaodai kuwa watoto wa kaka yake Gwajima, Faustine Mathias Gwajima, ambaye kwa sasa ni marehemu, wakimtaka askofu huyo kumfufua baba yao ndani ya siku 14 la sivyo watamfikisha mahakamani kwa kile walichokitaja kuwa amewasababishia athari kubwa za kisaikolojia kwa muda mrefu.

Wakizungumza mapema leo hii na waandishi wa habari Idara ya Habari Maelezo, Jijini Dar, watoto hao waliojitambulisha kwa majina ya Shamma Gwajima (18) na Raphah Gwajima (17) walisema kuwa baba yao ambaye ni kaka wa Askofu Gwajima alifariki dunia mwaka 2008 mkoani Mwanza kwa maradhi ambapo Askofu Gwajima wanayemwita baba mdogo alifika msibani hapo na kuwataka ndugu na marafiki waliokuwa wakiomboleza kifo cha mpendwa wao wasihuzunike kwa kuwa marehemu hakuwa amekufa bali amelala tu.

“Mchungaji Gwajima alitukataza tusilie na tusihofu kwa chochote kwa kuwa alikuwa na uwezo wa kumuombea marehemu hadi afufuke. Kauli hiyo ilitufanya tuanze kufurahi na akaushika mwili wa marehemu katikati ya umati wa watu na kuanza kuutikisa akimtaka baba yetu aamke lakini hakuamka,” alisema Shamma.

Watoto hao walidai kuwa tangu siku hiyo Gwajima aliondoka kimyakimya na kuingia mitini na kudai kuwa jambo hilo limewaathiri kihisia na kisaikolojia na wanajiandaa kumshtaki kutokana na usumbufu aliowasababishia katika kipindi kigumu cha msiba wa baba yao.

Watoto hao walienda mbali zaidi na kudai kuwa waliamua kukaa kimya wakiamini Askofu Gwajima ambaye ni baba yao mdogo anastahili heshima ya kichungaji mbele za watu, lakini walidai kuwa wanashangazwa na mambo ayafanyayo hivi karibuni kama vile kuwatukana watumishi wenzake na kutoa siri za waumini wanaoenda kwake kwa ajili ya kupata huduma za maombezi.

Aidha walidai kuwa Askofu Gwajima ni tapeli kwa kuwa anatumia huduma ya kufufua misukule ‘hewa’ kwa maslahi yake binafsi na kuitaka serikali iingilie kati kumchukulia hatua huku wakiitaka jamii isikubali udanganyifu wa askofu huyo kwa kuwa kama kweli anafufua watu basi angemfufua kaka yake.

“Je, misukule ambayo anatangaza ameifufua, tujiulize kabla ya kufariki ilikuwa ikiishi wapi? Na, je, kuna vyeti vya kifo vinavyothibitisha kama watu hao wanaofufuliwa walikufa kweli? Je, ndugu wa hiyo misukule wapo?” walisema watoto hao na kuongeza kuwa kutokana na kushindwa kwake kumfufua baba yao, Gwajima amewatelekeza kwa kutowapa msaada wowote licha ya yeye kuishi maisha ya kifahari.

VIJANA SITA WA JKT BULOMBORA KIGOMA MAPOTEZA MAISHA,21 WAJERUHIWA KATIKA AJALI

VIJANA sita waliokuwa katika mafunzo ya kijeshi ya kujitolea katika kikosi cha 821 JKT Bulombora mkoani Kigoma wamefariki dunia na wengine 21 kujeruhiwa vibaya kutokana na ajali ya gari iliyotokea jioni hii.
Mganga Mfawidhi wa hospital ya mkoa wa Kigoma Dkt. Fadhil Kibaya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
"Ni kweli leo majira ya saa moja jioni tumepokea miili minne ya vijana wa JKT ambao waliletwa hapa tayari wamefariki na majeruhi 21. "Wengine wawili wamefariki hapa hapa wakati tukiendelea kuwapa huduma"alisema Dkt Fadhili.
Alisema hali za majeruhi mpaka sasa siyo nzuri sana kwani wengi wameumia sehemu za kichwa na mwilini. "Bado tunaendelea na jitahada za kuwapatia matibabu na majina ya waliopoteza maisha pamoja majeruhi tutatoa kesho, sababu majeruhi wengi hawana fahamu"alisema.
Naye kamanda wa polisi mkoa wa kigoma Afande Ferdinand Mtui alisema chanzo cha ajali hiyo ni gari hilo la jeshi kushindwa kupanda mlima na kusababisha tairi mbili za nyuma kupasuka.
Alisema ajali hiyo imetokea katika eneo la Kasaka karibu na mizani ambapo lori hilo la jeshi lilikuwa likitoka mjini kwenda kambini likiwa limebeba makreti ya soda na unga.

KIMENUKA UPYA! Flora MBASHA Amburuza Tena Mumewe Mahakamani Siku Chache Baada Ya Kuachiwa Huru!

SIKU chache baada ya kushinda kesi ya tuhuma za kubaka iliyokuwa ikimkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, mwimbaji wa muziki wa Injili, Emmanuel Mbasha anatarajiwa kupandishwa tena katika korti hiyohiyo kwa madai mengine, Risasi Mchanganyiko lina habari kamili.
Mwimbaji wa muziki wa Injili, Emmanuel Mbasha.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni kwa sharti la kutotajwa jina, mmoja wa watu wa karibu na wanandoa hao, alisema Flora amefungua kesi ya madai ya talaka katika Mahakama ya Kisutu na kwamba muda si mrefu shauri hilo litaanza kusikilizwa.
“Flora ameenda mahakamani kudai talaka yake, kwa hiyo kesi inatarajiwa kuanza kusikilizwa muda wowote kuanzia sasa,” alisema mtoa habari huyo.Baada ya taarifa hizo, mwandishi wetu alimtafuta Mbasha kwa njia ya simu na kumuuliza juu ya madai hayo, ambapo alikiri na kudai anajiandaa kukabiliana na shitaka hilo. 
“Yeah, ni kweli kaka, Flora ameamua kwenda mahakamani kudai talaka yake, sioni kama ni tatizo, kwa sasa siwezi kuzungumza lolote kwa sababu limeshafika katika mkondo wa sheria na tunapaswa kusubiri tuone kitakachotokea, lakini naamini kila kitu kitakwenda sawa,” alisema Mbasha. 

Kwa upande wake, mke wa mwimbaji huyo, ambaye pia ni mkali wa nyimbo za gospo, Flora Mbasha alipotafutwa hakupokea simu yake ya mkononi, lakini alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms) alijibu kwa kifupi:
“Kaka, naendesha, kila kitu kiko mahakamani kwa hiyo sina la kuzungumza kwa sasa.”
Hali hiyo inatokea siku chache tu baada ya mahakama hiyo kumuachia huru mwimbaji huyo aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya ubakaji ambayo pia yalimleta mkewe huyo mahakamani akiwa shahidi wa upande wa mashtaka.
Kwa muda mrefu, waimbaji hao wamekuwa katika mgogoro wa kifamilia ambapo juhudi za watu mbalimbali zimefanyika kusuluhisha lakini hazikufanikiwa.

MZEE MAJUTO ASIMULIA ALIVYONUSURIKA HUKO MAKKA SAUDIA

Sstaa wa filamu za Kibongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto au King Majuto’ na baadhi ya mahujai.
Gladness Mallya BAADA ya kutokea vifo vya mahujaji zaidi ya mia saba waliokuwa wakishiriki Hija karibu na mji mtakatifu wa Waislam wa Makka, staa wa filamu za Kibongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto au King Majuto’ amesimulia alivyonusurika kwenye tukio hilo la kukanyagana.

Prof. Ibrahim Lipumba na baadhi ya mahujaji.
Akizungumza na gazeti hili mke wa Mzee Majuto, Aisha alisema baada ya kupata taarifa za mahujaji kufariki na mumewe alikuwa kwenye msafara huo alishtuka mno ambapo haraka alifanya mawasiliano naye na kumwelezea kwamba alinusurika na tukio hilo la kusikitisha.
Wahanga wa maafa ya mkanyagano kwenye hija mjini Makka, Saudi Arabia
“Nimeongea na Mzee Majuto kasema yuko vizuri na alinusurika kwenye mkanyagano huo kwani mahujaji walikuwa ni wengi sana ambapo walikuwa wakienda sehemu maalum kwa ajili ya kumpiga mawe shetani hivyo wakashindwa kupishana na kusababisha mkanyagano huo.

“Anasema alishuhudia watu walivyokuwa wakikanyagana ambapo wengine walijeruhiwa vibaya na vifo vikiwa ni vingi lakini anamshukuru Mungu amenusurika na tukio hilo baya na la kihistoria maishani mwake,” alisema Aisha.
Aliendelea kusema japokuwa mumewe amemhakikishia kwamba yuko salama lakini bado ana hofu kubwa mpaka sasa na kikubwa wanaendelea kumuombea kwa Mungu ili aweze kurudi salama.
“Yaani mpaka sasa tuna hofu kubwa mno, tunamuomba Mwenyezi Mungu amrudishe salama pia kwa mahujaji waliofariki tunamuomba Mwenyezi Mungu awaweke mahali pema peponi na ndugu zao tunawaombea faraja katika kipindi hiki kigumu,” alisema Aisha.
Mzee Majuto alikuwa ni miongoni mwa mahujaji waliokwenda Makka kwa ajili ya kuhiji ambapo mpaka Jumamosi vifo vya mahujaji vilikuwa vimefikia zaidi ya mia saba wakiwemo Watanzania watano.

VERY SHOCKING...JIONEE HII KALI MTANGAZAJI MAARUFU WA TV BONGO ANASWA 'AKIKATA GOGO' KWENYE DUST BIN MTAANI, BILA AIBUUU. JIONEE VIDEO HII HAPA===>>>

SHOCKING NEWS: KIRINYAGA School Girl With Bhang In Underwear Wants 5M Compensation

 week ago a bus was impounded by police in Kirinyaga when they got wind that it was ferrying students who were engaging in criminal activities.
And true to the wind that reached them, upon the impounding, it was discovered that the students were engaging in sex, smoking bhang and drinking alcohol as loud music boomed from the bus.
The graffiti on the bus also was very controversial as it encouraged the students to do unpalatable things.
But what happened after overshadowed the whole. One of the police officers who frisked the students went ahead to take photos of the school girl found hiding bhang in her underwear as she stood there semi-naked.
The police officer later circulated the photos on social media. This caused great anger among Kenyans who demanded for the prosecution of whoever took the photos. The officer has since been interdicted and is likely to face charges.
And now the girl whose photos were put on the internet has come out to allegedly demand 5M compensation.
SHOCKING NEWS: KIRINYAGA School Girl With Bhang In Underwear Wants 5M Compensation
SHOCKING NEWS: KIRINYAGA School Girl With Bhang In Underwear Wants 5M Compensation
Through her lawyer, Gladys Wamaitha, the school girl will petition inspector general of police and DPP Keriako Tobiko over the manner in which she was treated, Tuko reports.

HUYU NDIYE MCHUNGAJI ANAYEWALISHA WAUMINI WAKE NYOKA





TAZAMA MTOTO MZURI WA GADNER G HABASH, ALIVYO MKALI





www.CodeNirvana.in

Total Pageviews

Copyright © DAILY MAIL | Designed By Code Nirvana