Sexy lady wa filamu Bongo, Kajala Masanja akiwa na mwanaye Paula.
SEXY lady wa filamu Bongo, Kajala Masanja hivi karibuni aligeuka gumzo yeye na mwanaye walipoenda kufanya ‘shopping’ Mlimani City ambapo watu walikuwa wakiwakodolea macho kwa jinsi alivyolingana na mtoto wake.
Kajala alitinga eneo hilo na mtoto wake huyo aitwaye Paula ambapo awali walienda kupata chakula katika mgahawa wa SamakiSamaki na kisha waliingia ndani kwa ajili ya kufanya manunuzi mengine.
“Kwa kweli Kajala amekuza maana yeye na mtoto wake wamelingana sasa na mara nyingi kwa sasa hivi wanaongozana huku wakionekana kuwa na furaha wakati wote,” alisikika mtu mmoja akizungumza.
Post a Comment