Featured

    Featured Posts

Edward Lowassa Azidi Kukipasua Chama cha CCM...jionee Hapa.


Viongozi hao ni katibu wa zamani wa Itikadi na Uenezi wa mkoa wa Arusha, Issack Kapriano maarufu Kadogoo na Katibu wa zamani wa Uchumi na Fedha mkoa Kilimanjaro, Paul Matemu.
Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi, Loti Ole Nesele ametithibitishia jana kuwa Laizer kapewa likizo hadi baada ya uchaguzi.



Hata hivyo, chanzo cha habari cha uhakika kinasema, Kadogoo ambaye ana undugu na Laizer alimpigia simu ndugu yake huyo akimjulisha kuwa angepita Moshi akienda Mwanga, hivyo amsaidie kumwekea oda ya chakula, naye akafanya hivyo katika mgahawa wa East African ambapo walikutwa na kiongozi mmoja wa CCM.



Taarifa hizo zinadai siku iliyofuata, Laizer aliitwa na kuhojiwa na viongozi wa CCM, lakini akajitetea kuwa Kadogoo ni mjomba wake na asingeweza kumtenga kwa vile amehamia Chadema.
Laizer ni miongoni mwa wana- CCM waliokuwa wakimuunga mkono Lowassa wakati wa mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM.


Kutokana na tuhuma za kuendelea kushirikiana na mgombea huyo wa Ukawa, viongozi hao walipendekeza kwa uongozi wa mkoa wa Jumuiya hiyo umpe likizo ya lazima Laizer kwa siku 30, ili arejee baada ya Uchaguzi Mkuu kumalizika.


“Nimejiuliza maswali mengi lakini sipati majibu. Kwamba CCM imefika mahali inataka wana CCM wasichanganyikane na wafuasi wa vyama vingine. CCM wanataka kufanya siasa ni uadui?” alihoji.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM mkoa Kilimanjaro, Festo Kilawe, alipoulizwa kuhusu sakata hilo, aliomba aulizwe katibu wa jumuiya hiyo mkoa wa Kilimanjaro, Robert Chilamato.

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Total Pageviews

Copyright © DAILY MAIL | Designed By Code Nirvana