Kile kilio cha siku nyingi cha maumivu ya mkopo wa elimu ya juu kinakaribia kupatiwa jibu. Mgombea wa Urais wa CHADEMA/UKAWA Edward Lowassa ameahidi kuwasamehe wale wote waliokopeshwa na kodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB). Lowassa anamaanisha kuwa wanaodaiwa hawatalipa tena na itakuwa ni kama wamesomeshwa bure tu na Serikali yao.

Wakati huohuo, Lowassa anaendelea kusisitiza kuwa elimu ya chuo kikuu itakuwa bure. Wasomi wa wakati wa nyuma na wale wa sasa, mnataka nini tena? Lowassa, kutokana na ahadi zake za kiuchaguzi, anatamani kuona elimu inakuwa bure na hata wale waliokopeshwa wakijisikia kuwa wamesoma bure. Lengo kuu ni kutoa elimu ya bure na bora kwa maendeleo ya Tanzania yetu.

Mtampa kura wasomi wa Tanzania? Wale waliolipa hadi kumaliza mkopo, Serikali itawarudishia fedha zao? Tutege masikio tena kumsikia Lowassa atalisemeaje hili.