Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake Jeti Lumo, Dar es Salaam juzi, alisema hizo taarifa hizo si za kweli na ni uzushi.
“Mimi kama mwana familia nakanusha taarifa hizo zinazosambaa mitandaoni, habari hizo hazina ukweli hata kidogo.
Alisema ni kawaida kwa Jenerali Mwamunyange kumuaga kila anaposafiri na kama kaka yake alimuaga kuwa alikuwa anasafiri kikazi kwenda nje akianzia Italia.
Pia alikanusha taarifa zilizosema kuwa ukoo wao umepewa fedha kuzima taarifa za Jenerali Mwamunyange na akawataka wananchi kuzipuuza.
Post a Comment