Featured

    Featured Posts

TAZAMA MZEE YUSUPH ALIVYOWAPAGAWISHA WAPENDANAO DAR LIVE JANA

Mzee Yusuf akiwapagawisha mashabiki kwa wimbo wa My Valentine.
Muimbaji wa Jahazi, Leila akiimba Wimbo wa Fanya Yako.
Khadija Yusuf naye akiimba na mashabiki wimbo wake wa Hasidi Hana Sababu.
Mwansiti Mbwana akiwakonga na Wimbo wa Alipangalo Jalali.
Waimbaji wa Jahazi wakiwa katika picha ya pamoja.
Mashabiki wakimzunguka bi'dada (jina lake halikujulikana) akiyakata mauno.
Umati wa mashabiki wakipagawa na Jahazi Modern Taarab.
KUNDI linalotikisa kunako miondoko ya Pwani, Jahazi Modern Taarab likiongozwa na Mfalme Mzee Yusuf leo limefunika ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live katika shoo maalum ya Usiku wa Wapendanao 'Valentine's Day'.
Jahazi walianza kutawala jukwaa ambapo, Leila alikuwa wa kwanza kupanda na kuimba Wimbo wa Fanya Yako kisha akafuatiwa na Mwansiti na Fatuma Nyoro. Baadaye alipanda Mzee Yusuf kwa Wimbo wa My Valentine na kufanya ukumbi wote kulipuka kwa shangwe. Mzee Yusuf aliamsha shangwe zaidi baada ya kuimba Wimbo mpya wa Mahaba Niue.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Total Pageviews

Copyright © DAILY MAIL | Designed By Code Nirvana