![](http://api.ning.com/files/uoGx*LwXWSIOf35a44TqQ39c31g*R*rhe2N3PrRK9VhwOOZRq4WTfXkAJ*gPTOSnSC8Ew73ewmtq3HI1aAJbSivt2*uAAgOX/IMG_9816.jpg?width=450)
Mama mmoja ambaye jina lake hakupatikana mara moja, amefanya kituko cha mwaka baada ya kusaula mbele ya bintiye wa kumzaa, tukio ambalo limetafsiriwa kuwa ni mcharuko.
Tukio hilo la aibu lililoshuhudiwa na Risasi Jumamosi lilijiri katika Ukumbi wa Msasani Beach, jijini Dar hivi karibuni ambapo Akudo Impact ‘Vijana wa Masauti’ walikuwa wakimwaga burudani pande hizo.
Ishu yenyewe ilianza hivi; Awali mama huyo alionekana akizama kiwanjani hapo kwa mapozi ya kiungwana ambapo alifikika eneo hilo kwa kazi moja tu, yaani burudani.
![](http://api.ning.com/files/7E9Yy*jN1WKsOI-cfF-G1EpZN5aE3deVOf87RH1j3TEfTh4jgsyZ*J6v-7Y9VwYywgoD-Qdzw0Wku2r03juGRTMAAgOuzEGO/IMG_9771.jpg?width=359)
..mzuka haujapanda, niko poa tu!
Alipotia maguu tu ndani ya ukumbi huo, alivuta kiti na kuketi na mwanaye kisha kusoma mazingira kwanza kabla ya kuanza kufanya ‘mambo’.
Kama kawa, akiwa anasoma ‘mandhari’ ya ukumbi na bintiye, walikuwa wakikamua ‘matingasi babkubwa’ ambapo yalipokolea, ndipo ilipozaliwa stori hii.
![](http://api.ning.com/files/7E9Yy*jN1WJNYukKulRxo92NpOJVCacnHkioI-fzbSTbE13GrY*Z5caUAqmBF2ja6eJyIV0b*Y7oTC3bHkWco0zFubPHTWAF/IMG_9773.jpg?width=276)
..mtoto nae tayari yu mafunzoni..!
Haikupita ‘taimu’ kwani mzazi huyo alipotelewa na uungwana pale alipojikuta akisimama na kuanza kuserebuka sambamba na mwanaye.
Kadri mapigo ya Vijana wa Masauti yalivyozidi kuchanganya, ndivyo midadi ya ‘mtu mzima’ ilivyozidi kupanda na kuanza kukata kiuno isivyo kawaida huku akichojoa kiwalo kimoja baada ya kingine.
![](http://api.ning.com/files/uoGx*LwXWSIOf35a44TqQ39c31g*R*rhe2N3PrRK9VhwOOZRq4WTfXkAJ*gPTOSnSC8Ew73ewmtq3HI1aAJbSivt2*uAAgOX/IMG_9816.jpg?width=450)
...mzuka wangu ukinipanda......
Mzuka ulipokolea barabara, mama alijikuta akivua miwani yake ‘tintedi’ kwani ilikuwa ikimnyima raha kwa kutoona vizuri kwenye giza.
Baada ya miwani vilifuatia viatu, blauzi na kubakiza sidiria, huku chini akishusha ‘skini jinsi’ yake na kusababisha bikini na viungo nyeti kuwa nje nje mbele ya mwanaye aliyekuwa akiangalia pembeni kwa aibu kuu.
![](http://api.ning.com/files/H8Z281VintiZQvQKwiWKnFAO1pmqFbrVdKXx9snP0p8i-wM3wfMEsvH3IUf347peYgDXlwguJgRp9CN9Aw5d-Ct5AJ0q3-la/IMG_9822.jpg?width=280)
...hata nguo huwa navua...!
Mizuka ya mama huyo ilishindwa kutulizwa mpaka wasamaria walipoamrisha Vijana wa Masauti kuzima muziki ndipo mzazi huyo akatulia na kwenda kukaa huku watu wakimponda kwa kitendo chake cha kumwaga radhi mbele ya mwanaye. Baadaye alitimkia kusikojulikana huku mtoto akielekeza njia tofauti na walipoingia kwani mama ndiye aliyekuwa ‘dairekta’.
Post a Comment